Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Hosea 13:1-6

Hosea 13:1-6 NENO

Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka; alitukuzwa katika Israeli. Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali, naye akafa. Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi; wanajitengenezea sanamu kutokana na fedha yao, vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari, vyote kazi ya fundi stadi. Inasemekana kuhusu hawa watu, “Hutoa dhabihu za binadamu na kubusu sanamu za ndama.” Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao, kama makapi yapeperushwayo kutoka sakafu ya kupuria nafaka, kama moshi utorokao kupitia dirishani. “Bali mimi ndimi BWANA Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi. Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo. Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.