Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mwanzo 33:12-20

Mwanzo 33:12-20 NENO

Ndipo Esau akasema, “Tuendelee na safari; nitakusindikiza.” Lakini Yakobo akamwambia, “Bwana wangu, unajua kwamba watoto ni wachanga na kwamba ni lazima nitunze hawa ngʼombe na kondoo wanaonyonyesha. Wakipelekwa kwa haraka hata kama ni kwa siku moja tu, wanyama wote watakufa. Hivyo bwana wangu, mtangulie mtumishi wako, nami nije polepole kwa mwendo wa makundi yaliyo mbele yangu na mwendo wa watoto, hadi nifike kwa bwana wangu huko Seiri.” Esau akamwambia, “Basi kubali nikuachie baadhi ya watu wangu.” Yakobo akauliza, “Lakini kwa nini ufanye hivyo? Niache tu nipate kibali machoni pa bwana wangu.” Hivyo siku hiyo Esau akashika njia, akarudi Seiri. Pamoja na hayo, Yakobo akaenda Sukothi. Akajijengea makazi na pia vibanda vya mifugo yake. Hii ndiyo sababu mahali pale panaitwa Sukothi. Baada ya Yakobo kutoka Padan-Aramu, alifika salama katika mji wa Shekemu huko Kanaani, na kuweka kambi yake karibu na mji huo. Akanunua kiwanja kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa bei ya vipande mia moja vya fedha, akapiga hema lake hapo. Akajenga madhabahu pale na kupaita El-Elohe-Israeli.