Ezekieli 20:45-49
Ezekieli 20:45-49 NENO
Neno la BWANA likanijia kusema: “Mwanadamu, uelekeze uso wako upande wa kusini, hubiri dhidi ya upande wa kusini, na utoe unabii dhidi ya msitu wa Negebu. Waambie watu wa Negebu: ‘Sikieni neno la BWANA. Hili ndilo asemalo BWANA Mwenyezi: Ninakaribia kukuwasha moto, nao utateketeza miti yako yote, mibichi na iliyokauka. Miali ya moto haitaweza kuzimwa na kila uso kutoka kusini mpaka kaskazini utakaushwa kwa moto huo. Kila mmoja ataona kuwa Mimi BWANA ndiye niliyeuwasha huo moto; nao hautazimwa.’ ” Ndipo niliposema, “Aa, BWANA Mwenyezi! Wao hunisema, ‘Huyu si huzungumza mafumbo tu?’ ”