1
Mateo 14:30-31
Swahili Roehl Bible 1937
SRB37
Lakini alipotazama, upepo ulivyo na nguvu, akaogopa, akaanza kuzama majini, akapiga kelele akisema: Bwana, niokoa! Mara Yesu akaunyosha mkono, akamshika, akamwambia: Mbona unanitegemea kidogo tu? Mbona umeingiwa na wasiwasi?
Linganisha
Chunguza Mateo 14:30-31
2
Mateo 14:30
Lakini alipotazama, upepo ulivyo na nguvu, akaogopa, akaanza kuzama majini, akapiga kelele akisema: Bwana, niokoa!
Chunguza Mateo 14:30
3
Mateo 14:27
Papo hapo Yesu akawaambia akisema: Tulieni! Ni miye, msiogope!
Chunguza Mateo 14:27
4
Mateo 14:28-29
Petero akamjibu akisema: Bwana, ukiwa ni wewe, agiza nije kwako majini juujuu! Alipomwambia: Njoo! Petero akashuka chomboni, akaenda juu ya maji, amfikie Yesu.
Chunguza Mateo 14:28-29
5
Mateo 14:33
Nao waliokuwamo chomboni wakamwangukia wakisema: Kweli ndiwe Mwana wa Mungu!
Chunguza Mateo 14:33
6
Mateo 14:16-17
Yesu akawaambia: Waendeje? Wapeni ninyi vyakula! Nao wakamwambia: Hatuna kitu hapa ila mikate mitano na visamaki viwili.
Chunguza Mateo 14:16-17
7
Mateo 14:18-19
Naye akasema: Nileteeni hapa! Akawaagiza hao watu wengi, wakae chini majanini. Akaitwaa ile mikate mitano na vile visamaki viwili, akatazama juu mbinguni akaviombea, akawamegea, akawapa wanafunzi ile mikate; nao wanafunzi wakawapa wale watu wengi.
Chunguza Mateo 14:18-19
8
Mateo 14:20
Wakala wote, wakashiba. Kisha wakayaokota makombo ya mikate yaliyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
Chunguza Mateo 14:20
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video