1
Wafilipi 4:6
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
TKU
Msisumbuke kitu chochote, lakini salini na kumwomba Mungu kwa mahitaji yenu. Mshukuruni Mungu wakati mnapomwomba yale mnayohitaji.
Linganisha
Chunguza Wafilipi 4:6
2
Wafilipi 4:7
Na kwa kuwa ninyi ni milki ya Kristo Yesu, amani ya Mungu itailinda mioyo na mawazo yenu isipate wasiwasi. Amani yake inaweza kutenda haya zaidi ya akili za kibinadamu.
Chunguza Wafilipi 4:7
3
Wafilipi 4:8
Na sasa, mwisho kabisa, kaka na dada zangu, fikirini kuhusu yale yaliyo ya kweli, ya kuheshimiwa, ya haki, yaliyo safi, yenye kupendeza, na yanayosemwa vema.
Chunguza Wafilipi 4:8
4
Wafilipi 4:13
Kristo ndiye anayenitia nguvu kuyakabili mazingira yote katika maisha.
Chunguza Wafilipi 4:13
5
Wafilipi 4:4
Furahini katika Bwana daima. Ninasema tena, furahini.
Chunguza Wafilipi 4:4
6
Wafilipi 4:19
Mungu wangu atatumia utajiri wake wenye utukufu kuwapa ninyi kila kitu mnachohitaji kupitia Kristo Yesu.
Chunguza Wafilipi 4:19
7
Wafilipi 4:9
Yatendeni yale mliyojifunza na kupokea kutoka kwangu, niliyowaambia na yale mliyoyaona nikitenda. Na Mungu atoaye amani atakuwa pamoja nanyi.
Chunguza Wafilipi 4:9
8
Wafilipi 4:5
Kila mtu auone wema na uvumilivu wenu. Bwana yu karibu kuja.
Chunguza Wafilipi 4:5
9
Wafilipi 4:12
Ninajua namna ya kuishi ninapokuwa na vichache na ninapokuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuishi katika hali zote, ninapokuwa na vyakula vingi au ninapokuwa na njaa, ninapokuwa na vingi zaidi ya ninavyohitaji au ninapokuwa sina kitu.
Chunguza Wafilipi 4:12
10
Wafilipi 4:11
Ninawaambia hili, si kwa sababu ninahitaji msaada kutoka kwa yeyote. Nimejifunza kuridhika na kile nilichonacho na chochote kinachotokea.
Chunguza Wafilipi 4:11
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video