Ufunuo 9:20-21
Ufunuo 9:20-21 SWC02
Watu waliobaki bila kuuawa na yale mapigo hawakuachana na sanamu walizojitengenezea wao wenyewe. Hawakuacha kuabudu pepo, sanamu za zahabu, za feza, za shaba, za mawe na za miti zisizoweza kuona, wala kusikia, wala kutembea. Watu wale hawakuacha hata matendo yao ya uuaji, ya uchawi, ya uasherati na ya wizi.





