YouVersion Logo
Search Icon

Ufunuo 14:9-11

Ufunuo 14:9-11 SWC02

Na malaika wa tatu akafuata wale wawili wa kwanza, akisema kwa sauti kubwa: “Kila mutu anayeabudu yule nyama na sanamu yake na kupigwa chapa juu ya paji la uso wake au juu ya mukono wake, naye vilevile atakunywa divai kali ya hasira ya Mungu iliyotengenezwa pasipo kuchangwa na maji na kumimiwa ndani ya kikombe chenye kujaa kasirani yake! Na watu kama wale, watateswa ndani ya moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto mbele ya wamalaika watakatifu na mbele ya Mwana- Kondoo. Na moshi wa ule moto wa mateso yao utakuwa ukipanda juu kwa milele na milele. Wale walioabudu yule nyama na sanamu yake na mutu yeyote aliyepigwa chapa ya jina lake, hawatapumzika hata siku moja usiku na muchana.”