Ufunuo 10:9-10
Ufunuo 10:9-10 SWC02
Nami nikaenda karibu na yule malaika, nikamwomba anipe kile kitabu kidogo. Naye akaniambia: “Ukitwae na ukikule, kitakuwa uchungu katika tumbo lako, lakini kitakuwa kitamu kama asali ndani ya kinywa chako.” Basi nikatwaa kitabu kile kidogo toka katika mukono wake, nikakikula. Kikakuwa kitamu kama asali ndani ya kinywa changu, lakini wakati nilipokimeza, nikasikia uchungu ndani ya tumbo langu.





