Zaburi 30
30
Maombi ya shukrani
1Mashairi yanayoelekea muzinduo wa hekalu. Zaburi ya Daudi.
2Ninakutukuza,
ee Yawe,
maana umeniokoa,
wala haukuwaacha waadui zangu wanisimange.
3Ee Yawe, Mungu wangu,
nilikulilia, nawe ukaniponyesha.
4Ee Yawe, umeniokoa kutoka kuzimu;
umenipa tena uzima,
umenitoa kutoka kati ya wafu.
5Mumwimbie Yawe sifa, enyi waaminifu wake;
mukumbuke utakatifu wake na kumushukuru.
6Hasira yake inadumu muda kidogo tu,
upendo wake unadumu milele.
Kilio kinaweza kuwa usiku,
lakini muchana kunatokea furaha.
7Mimi nilipofanikiwa, nilisema:
“Sitashindwa hata kidogo!
8Kwa upendo wako, ee Yawe,
umeniimarisha kama mulima mukubwa.”
Lakini ukajificha mbali nami,
nami nikafazaika.
9Nilikulilia wewe, ee Yawe;
nilikusihi, ee Yawe:
10“Utapata faida gani nikikufa
na kushuka mpaka katika shimo la wafu?
Mavumbi ya wafu yanaweza kukusifu?
Yanaweza kusimulia uaminifu wako?
11Usikie, ee Yawe, unihurumie;
ee Yawe, unisaidie!”
12Wewe umegeuza malalamiko yangu kuwa ngoma ya furaha;
umeniondolea huzuni yangu, ukanijaza furaha.
13Mimi nitakusifu wala sitakaa kimya.
Ee Yawe, Mungu wangu, nitakushukuru milele.
Currently Selected:
Zaburi 30: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Zaburi 30
30
Maombi ya shukrani
1Mashairi yanayoelekea muzinduo wa hekalu. Zaburi ya Daudi.
2Ninakutukuza,
ee Yawe,
maana umeniokoa,
wala haukuwaacha waadui zangu wanisimange.
3Ee Yawe, Mungu wangu,
nilikulilia, nawe ukaniponyesha.
4Ee Yawe, umeniokoa kutoka kuzimu;
umenipa tena uzima,
umenitoa kutoka kati ya wafu.
5Mumwimbie Yawe sifa, enyi waaminifu wake;
mukumbuke utakatifu wake na kumushukuru.
6Hasira yake inadumu muda kidogo tu,
upendo wake unadumu milele.
Kilio kinaweza kuwa usiku,
lakini muchana kunatokea furaha.
7Mimi nilipofanikiwa, nilisema:
“Sitashindwa hata kidogo!
8Kwa upendo wako, ee Yawe,
umeniimarisha kama mulima mukubwa.”
Lakini ukajificha mbali nami,
nami nikafazaika.
9Nilikulilia wewe, ee Yawe;
nilikusihi, ee Yawe:
10“Utapata faida gani nikikufa
na kushuka mpaka katika shimo la wafu?
Mavumbi ya wafu yanaweza kukusifu?
Yanaweza kusimulia uaminifu wako?
11Usikie, ee Yawe, unihurumie;
ee Yawe, unisaidie!”
12Wewe umegeuza malalamiko yangu kuwa ngoma ya furaha;
umeniondolea huzuni yangu, ukanijaza furaha.
13Mimi nitakusifu wala sitakaa kimya.
Ee Yawe, Mungu wangu, nitakushukuru milele.
Currently Selected:
:
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.