Zaburi 24
24
Mufalme Mukubwa
1Zaburi ya Daudi.
Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Yawe;
ulimwengu na wote wanaoishi ndani yake ni mali yake. #Ang. 1 Kor 10.26
2Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari;
aliisimika imara juu ya maji mengi.
3Nani atakayepanda kwa mulima wa Yawe?
Nani atakayekaa katika hekalu lake takatifu?
4Ni mutu wa matendo mema na moyo safi,
asiyefuata mambo ya ovyo,
wala kuapa kwa uongo. #Ang. Mat 5.8
5Mutu huyo atapokea baraka kwa Yawe,
na haki yake kwa Mungu mwokozi wake.
6Ndiyo hali ya kizazi cha watu wanaomutafuta yeye,
watu wanaomutafuta Mungu wa Yakobo.
7Mufunguke, enyi milango;
mufunguke, enyi milango ya tangia zamani,
kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie.
8Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu?
Ni Yawe, mwenye nguvu na uwezo;
Yawe, mwenye uwezo katika vita.
9Mufunguke, enyi milango,
mufunguke, enyi milango ya tangia zamani,
kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie.
10Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu?
Ni Yawe, wa majeshi,
yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu.
Currently Selected:
Zaburi 24: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Zaburi 24
24
Mufalme Mukubwa
1Zaburi ya Daudi.
Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Yawe;
ulimwengu na wote wanaoishi ndani yake ni mali yake. #Ang. 1 Kor 10.26
2Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari;
aliisimika imara juu ya maji mengi.
3Nani atakayepanda kwa mulima wa Yawe?
Nani atakayekaa katika hekalu lake takatifu?
4Ni mutu wa matendo mema na moyo safi,
asiyefuata mambo ya ovyo,
wala kuapa kwa uongo. #Ang. Mat 5.8
5Mutu huyo atapokea baraka kwa Yawe,
na haki yake kwa Mungu mwokozi wake.
6Ndiyo hali ya kizazi cha watu wanaomutafuta yeye,
watu wanaomutafuta Mungu wa Yakobo.
7Mufunguke, enyi milango;
mufunguke, enyi milango ya tangia zamani,
kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie.
8Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu?
Ni Yawe, mwenye nguvu na uwezo;
Yawe, mwenye uwezo katika vita.
9Mufunguke, enyi milango,
mufunguke, enyi milango ya tangia zamani,
kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie.
10Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu?
Ni Yawe, wa majeshi,
yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu.
Currently Selected:
:
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.