Zaburi 142
142
Maombi ya mutu aliyeachwa pekee
1Mashairi ya Daudi alipokuwa ndani ya pango.
2Ninamulilia Yawe kwa sauti kubwa,
ninamusihi Yawe kwa sauti kubwa.
3Ninamutolea malalamiko yangu,
ninamwelezea taabu zangu.
4Roho yangu inaporegea kabisa,
yeye yuko, anajua mwenendo wangu.
Waadui wamenitegea mitego katika njia ninayopita.
5Nikiangalia kwa kuume kwangu na kungojea,
ninaona hakuna mutu wa kunisaidia;
sina tena nafasi ya kukimbilia,
hakuna mutu anayenijali.
6Ninakulilia wewe, ee Yawe!
Wewe ni kimbilio langu;
wewe ni hitaji langu lote katika inchi ya wenye uzima.
7Usikilize kilio changu, maana nimetabanika sana;
uniokoe kutoka watesaji wangu, maana wamenizidi nguvu.
8Uniondoe humu katika kifungo,
kusudi nipate kukushukuru,
nikijiunga na watu wa haki
kwa sababu ya vyote ulivyonitendea.
Currently Selected:
Zaburi 142: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Zaburi 142
142
Maombi ya mutu aliyeachwa pekee
1Mashairi ya Daudi alipokuwa ndani ya pango.
2Ninamulilia Yawe kwa sauti kubwa,
ninamusihi Yawe kwa sauti kubwa.
3Ninamutolea malalamiko yangu,
ninamwelezea taabu zangu.
4Roho yangu inaporegea kabisa,
yeye yuko, anajua mwenendo wangu.
Waadui wamenitegea mitego katika njia ninayopita.
5Nikiangalia kwa kuume kwangu na kungojea,
ninaona hakuna mutu wa kunisaidia;
sina tena nafasi ya kukimbilia,
hakuna mutu anayenijali.
6Ninakulilia wewe, ee Yawe!
Wewe ni kimbilio langu;
wewe ni hitaji langu lote katika inchi ya wenye uzima.
7Usikilize kilio changu, maana nimetabanika sana;
uniokoe kutoka watesaji wangu, maana wamenizidi nguvu.
8Uniondoe humu katika kifungo,
kusudi nipate kukushukuru,
nikijiunga na watu wa haki
kwa sababu ya vyote ulivyonitendea.
Currently Selected:
:
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.