Matayo 28:12-15
Matayo 28:12-15 SWC02
Wakubwa wa makuhani wakakutana pamoja na wasimamizi wa watu na kukata shauri. Wakawapa wale waaskari feza nyingi wakiwaambia: “Mutasema kwamba wanafunzi wake walikuja kuiba maiti yake usiku wakati mulipokuwa mukilala usingizi. Na kama liwali akisikia habari hii, sisi tutasemezana naye na kuhakikisha yale yaliyotokea kusudi musipate matata.” Basi wale waaskari walinzi wakapokea zile feza na kufanya sawa walivyoambiwa. Na habari hii ilienea katikati ya Wayuda mpaka leo.





