Yobu 12
12
1Halafu Yobu akajibu:
2Hakika! Ninyi ni watu wa hekima.
Hekima itakufa wakati ule mutakapokufa.
3Mimi nami nina ufahamu kama ninyi.
Mimi si mutu wa akili ndogo kuliko ninyi.
Yote muliyosema kila mutu anajua.
4Nilikuwa mutu wa kumwomba Mungu na kupata jibu lake.
Sasa, watu wananichekelea.
Wanachekelea mutu mukamilifu, mwenye haki.
5Mutu mwenye raha anazarau taabu;
taabu ni kwa wale wanaoteleza.
6Makao ya wanyanganyi yana amani.
Wenye kumuchokoza Mungu wako salama;
nguvu yao ni mungu wao.
7Lakini uulize nyama nao watakufundisha;
uulize ndege nao watakuambia.
8Au uulize mimea nayo itakufundisha;
sema na samaki nao watakuarifu.
9Nani kati ya viumbe hivyo,
asiyejua kwamba Yawe ametenda yale?
10Uzima wa kila kiumbe,
pumzi ya kila mwanadamu,
viko katika mikono yake.
11Sikio halipimi maneno
kama vile ulimi unavyoonja chakula?
12Hekima iko kwa watu wazee,
maarifa kwa walioishi muda murefu.
13Lakini hekima na uwezo ni vya Mungu.
Yeye ana maarifa na ujuzi.
14Akibomoa, hakuna anayeweza kujenga upya;
akifunga mutu, hakuna anayeweza kumufungua.
15Akizuia mvua, inchi inakauka;
akiifungulia, inchi inaharibika.
16Yeye ana nguvu na hekima.
Wanaodanganywa na wanaodanganya ni wake.
17Anawatembeza washauri miguu wazi,
anawafanya waamuzi kuwa wapumbafu.
18Anavua wafalme mikaba yao,
na kuwafunga kamba za wafungwa katika viuno.
19Anaacha makuhani watembee uchi;
na kuwaangusha wenye nguvu.
20Ananyanganya washauri zawadi yao ya kusema,
anaondolea wazee ufahamu wao.
21Anamwagia wakubwa mazarau,
anawaondolea wenye uwezo nguvu yao.
22Anafunua vilindi vya giza,
na kuleta katika mwangaza mambo yaliyokuwa katika giza.
23Anayaongeza mataifa kisha anayaangamiza,
anayafanya yapanuke kisha anayatawanya.
24Anaondolea viongozi wa watu ujuzi wao,
anawafanya watangetange katika jangwa kusikokuwa njia,
25wakipapasapapasa katika giza kusikokuwa mwangaza;
na kuwafanya wapepesuke kama walevi.
Jibu la Yobu linaendelea
Currently Selected:
Yobu 12: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Yobu 12
12
1Halafu Yobu akajibu:
2Hakika! Ninyi ni watu wa hekima.
Hekima itakufa wakati ule mutakapokufa.
3Mimi nami nina ufahamu kama ninyi.
Mimi si mutu wa akili ndogo kuliko ninyi.
Yote muliyosema kila mutu anajua.
4Nilikuwa mutu wa kumwomba Mungu na kupata jibu lake.
Sasa, watu wananichekelea.
Wanachekelea mutu mukamilifu, mwenye haki.
5Mutu mwenye raha anazarau taabu;
taabu ni kwa wale wanaoteleza.
6Makao ya wanyanganyi yana amani.
Wenye kumuchokoza Mungu wako salama;
nguvu yao ni mungu wao.
7Lakini uulize nyama nao watakufundisha;
uulize ndege nao watakuambia.
8Au uulize mimea nayo itakufundisha;
sema na samaki nao watakuarifu.
9Nani kati ya viumbe hivyo,
asiyejua kwamba Yawe ametenda yale?
10Uzima wa kila kiumbe,
pumzi ya kila mwanadamu,
viko katika mikono yake.
11Sikio halipimi maneno
kama vile ulimi unavyoonja chakula?
12Hekima iko kwa watu wazee,
maarifa kwa walioishi muda murefu.
13Lakini hekima na uwezo ni vya Mungu.
Yeye ana maarifa na ujuzi.
14Akibomoa, hakuna anayeweza kujenga upya;
akifunga mutu, hakuna anayeweza kumufungua.
15Akizuia mvua, inchi inakauka;
akiifungulia, inchi inaharibika.
16Yeye ana nguvu na hekima.
Wanaodanganywa na wanaodanganya ni wake.
17Anawatembeza washauri miguu wazi,
anawafanya waamuzi kuwa wapumbafu.
18Anavua wafalme mikaba yao,
na kuwafunga kamba za wafungwa katika viuno.
19Anaacha makuhani watembee uchi;
na kuwaangusha wenye nguvu.
20Ananyanganya washauri zawadi yao ya kusema,
anaondolea wazee ufahamu wao.
21Anamwagia wakubwa mazarau,
anawaondolea wenye uwezo nguvu yao.
22Anafunua vilindi vya giza,
na kuleta katika mwangaza mambo yaliyokuwa katika giza.
23Anayaongeza mataifa kisha anayaangamiza,
anayafanya yapanuke kisha anayatawanya.
24Anaondolea viongozi wa watu ujuzi wao,
anawafanya watangetange katika jangwa kusikokuwa njia,
25wakipapasapapasa katika giza kusikokuwa mwangaza;
na kuwafanya wapepesuke kama walevi.
Jibu la Yobu linaendelea
Currently Selected:
:
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.