Yeremia 47
47
Neno la Yawe juu ya Wafilistini
Misri inashambuliwa
1Hili ni neno Yawe alilomwambia nabii Yeremia juu ya Wafilistini, mbele mufalme wa Misri hajaushambulia muji wa Gaza:
2Yawe anasema hivi:
Maji yanapanda kutoka kaskazini,
nayo yatakuwa muto uliofurika;
yataifunika inchi nzima na vyote vinavyokuwa ndani yake,
muji na wakaaji na wanaoishi humo.
Watu watalia,
wakaaji wote wa inchi wataomboleza.
3Watasikia shindo la kwato za farasi,
kelele za magari ya vita,
na vishindo vya magurudumu yao.
Wababa watawasahau watoto wao,
mikono yao itakuwa imeregea sana.
4Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilistini wote,
kukomesha musaada uliobakia kutoka Tiro na Sidona.
Maana Yawe anawaangamiza Wafilistini,
watu waliobaki wa kisanga cha Kafutori.
5Watu wa Gaza wamenyoa kichwa kwa kuomboleza;
muji wa Askeloni umeangamia.
Enyi watu muliobaki katika bonde
mutajikatakata kwa huzuni mpaka wakati gani?
6Ee upanga wa Yawe!
Utatwaa muda gani ndipo utulie?
Ingia katika mufuko wako,
upate kutulia na kunyamaza!
7Lakini utaweza kutulia namna gani,
ikiwa ni Yawe ameupa kazi?
Ameuamuru ushambulie muji wa Askeloni
na watu wanaoishi kandokando ya bahari.
Currently Selected:
Yeremia 47: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Yeremia 47
47
Neno la Yawe juu ya Wafilistini
Misri inashambuliwa
1Hili ni neno Yawe alilomwambia nabii Yeremia juu ya Wafilistini, mbele mufalme wa Misri hajaushambulia muji wa Gaza:
2Yawe anasema hivi:
Maji yanapanda kutoka kaskazini,
nayo yatakuwa muto uliofurika;
yataifunika inchi nzima na vyote vinavyokuwa ndani yake,
muji na wakaaji na wanaoishi humo.
Watu watalia,
wakaaji wote wa inchi wataomboleza.
3Watasikia shindo la kwato za farasi,
kelele za magari ya vita,
na vishindo vya magurudumu yao.
Wababa watawasahau watoto wao,
mikono yao itakuwa imeregea sana.
4Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilistini wote,
kukomesha musaada uliobakia kutoka Tiro na Sidona.
Maana Yawe anawaangamiza Wafilistini,
watu waliobaki wa kisanga cha Kafutori.
5Watu wa Gaza wamenyoa kichwa kwa kuomboleza;
muji wa Askeloni umeangamia.
Enyi watu muliobaki katika bonde
mutajikatakata kwa huzuni mpaka wakati gani?
6Ee upanga wa Yawe!
Utatwaa muda gani ndipo utulie?
Ingia katika mufuko wako,
upate kutulia na kunyamaza!
7Lakini utaweza kutulia namna gani,
ikiwa ni Yawe ameupa kazi?
Ameuamuru ushambulie muji wa Askeloni
na watu wanaoishi kandokando ya bahari.
Currently Selected:
:
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.