Isaya 17
17
Mungu ataazibu Asuria na Israeli
1Ujumbe wa Mungu juu ya muji wa Damasiki.
Damasiki utakoma kuwa muji;
utakuwa lundo la mabomoko. #Ang. Yer 49.23-27; Amo 1.3-5; Zak 9.1
2Miji inayokuwa chini yake imeachwa matongo milele.
Itakuwa makao ya makundi ya nyama,
wala hakuna mutu atakayewatisha.
3Pango za Efuraimu zitatoweka,
na utawala wa Damasiki utakwisha.
Waaramu ambao watabaki wazima,
hawatakuwa na utukufu zaidi kama wazao wa Israeli.
–Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.
Watakaobaki katika Israeli
4Siku hiyo, utukufu wa Yakobo utaporomoshwa,
na unono wake utapotea.
5Itakuwa kama wakati wa mavuno,
wakati wamekwisha kuokota ngano,
na kukusanya masuke katika mukono.
Hakika, itakuwa kama bonde la Refaimu
wakati wamekwisha kuvuna ngano.
6Watabaki wachache kama vile kisha kuangusha matunda ya mizeituni:
matunda mawili au matatu katika tawi la juu;
mane, matano katika matawi yanayozaa sana.
–Ni ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli.
Mwisho wa kuabudu sanamu
7Siku hiyo, watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa huyo Mutakatifu wa Israeli. 8Hawataelekea tena mazabahu ambazo ni kazi za vidole vyao wenyewe, wala kuzitazamia tena kazi za mikono yao wenyewe, ni kusema sanamu za mungu Ashera na mazabahu za kufukizia ubani.
9Siku hiyo miji yao imara itaachwa matongo, kama miji ambayo Wahivi na Waamori waliihama walipokuwa wakiwakimbia wazao wa Israeli. Kila kitu kitakuwa uharibifu.
10Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa,
haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia.
Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali,#17.10 ya Bali: neno kwa neno: “ya yule muzuri”; labda jina la sifa la Bali.
na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;
11hata mukiifanya ikomae siku hiyohiyo muliyoipanda
na kuifanya ichanue asubui hiyohiyo,
mavuno yenu yatatoweka
siku hiyo ya hasara na maumivu yasiyoweza kuponyeshwa.
Mataifa adui yanashindwa
12Aha! Ngurumo ya watu wengi!
Wananguruma kama bahari.
Aha! Mulio wa watu wa mataifa!
Yanatoa mulio kama wa maji mengi.
13Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi,
lakini Mungu atayakaripia, nayo yatakimbilia mbali.
Yatafukuzwa kama maganda juu ya mulima mbele ya upepo;
kama mavumbi yanayonyanyuliwa na upepo mukali.
14Wakati wa magaribi yanaleta hofu kubwa,
lakini mbele ya asubui yametoweka!
Ndilo litakalowapata wale wanaotukamata
na kutunyanganya mali yetu.
Currently Selected:
Isaya 17: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Isaya 17
17
Mungu ataazibu Asuria na Israeli
1Ujumbe wa Mungu juu ya muji wa Damasiki.
Damasiki utakoma kuwa muji;
utakuwa lundo la mabomoko. #Ang. Yer 49.23-27; Amo 1.3-5; Zak 9.1
2Miji inayokuwa chini yake imeachwa matongo milele.
Itakuwa makao ya makundi ya nyama,
wala hakuna mutu atakayewatisha.
3Pango za Efuraimu zitatoweka,
na utawala wa Damasiki utakwisha.
Waaramu ambao watabaki wazima,
hawatakuwa na utukufu zaidi kama wazao wa Israeli.
–Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.
Watakaobaki katika Israeli
4Siku hiyo, utukufu wa Yakobo utaporomoshwa,
na unono wake utapotea.
5Itakuwa kama wakati wa mavuno,
wakati wamekwisha kuokota ngano,
na kukusanya masuke katika mukono.
Hakika, itakuwa kama bonde la Refaimu
wakati wamekwisha kuvuna ngano.
6Watabaki wachache kama vile kisha kuangusha matunda ya mizeituni:
matunda mawili au matatu katika tawi la juu;
mane, matano katika matawi yanayozaa sana.
–Ni ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli.
Mwisho wa kuabudu sanamu
7Siku hiyo, watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa huyo Mutakatifu wa Israeli. 8Hawataelekea tena mazabahu ambazo ni kazi za vidole vyao wenyewe, wala kuzitazamia tena kazi za mikono yao wenyewe, ni kusema sanamu za mungu Ashera na mazabahu za kufukizia ubani.
9Siku hiyo miji yao imara itaachwa matongo, kama miji ambayo Wahivi na Waamori waliihama walipokuwa wakiwakimbia wazao wa Israeli. Kila kitu kitakuwa uharibifu.
10Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa,
haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia.
Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali,#17.10 ya Bali: neno kwa neno: “ya yule muzuri”; labda jina la sifa la Bali.
na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;
11hata mukiifanya ikomae siku hiyohiyo muliyoipanda
na kuifanya ichanue asubui hiyohiyo,
mavuno yenu yatatoweka
siku hiyo ya hasara na maumivu yasiyoweza kuponyeshwa.
Mataifa adui yanashindwa
12Aha! Ngurumo ya watu wengi!
Wananguruma kama bahari.
Aha! Mulio wa watu wa mataifa!
Yanatoa mulio kama wa maji mengi.
13Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi,
lakini Mungu atayakaripia, nayo yatakimbilia mbali.
Yatafukuzwa kama maganda juu ya mulima mbele ya upepo;
kama mavumbi yanayonyanyuliwa na upepo mukali.
14Wakati wa magaribi yanaleta hofu kubwa,
lakini mbele ya asubui yametoweka!
Ndilo litakalowapata wale wanaotukamata
na kutunyanganya mali yetu.
Currently Selected:
:
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.