Hosea 6
6
Musamaha usiokuwa wa kweli
1Halafu watasema: Tuende tumurudilie Yawe!
Yeye mwenyewe ameturarua,
lakini yeye mwenyewe atatuponyosha.
Yeye mwenyewe ametuumiza,
lakini yeye mwenyewe atatunza vidonda.
2Nyuma ya siku mbili atatupatia tena uzima.
Nyuma ya siku tatu atatufufua
kusudi tuweze kuishi pamoja naye.
3Basi tumutambue,
tujikaze sana kumujua Yawe.
Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko,
yeye atatufikia kama vile manyunyu,
kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.
4Lakini Yawe anasema hivi:
Nitakutendea nini, ee Efuraimu?
Nikufanyie nini, ee Yuda?
Upendo wenu kwangu ni kama ukungu wa asubui,
kama umande unaotoweka upesi.
5Ndiyo maana ninawashambulia kwa njia ya manabii,
nimewaangamiza kwa maneno yangu,
hukumu yangu inajitokeza kama mapambazuko.
6Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka,
kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.
Maovu yanaenea katika inchi yote
7Lakini mulivunja agano langu
kama mulivyofanya katika muji wa Adamu;
kule walikosa uaminifu kwangu.
8Gileadi ni muji wa waovu,
umejaa damu.
9Kama vile wanyanganyi wanavyomuvizia mutu katika njia,
ndivyo makuhani walivyojikusanya na kuvizia.
Wanaua watu katika njia yenye kuelekea Sekemu,
na kutenda uovu mukubwa.
10Nimeona jambo la kuchukiza sana
kati ya Waisraeli:
watu wa Efuraimu wanakimbilia miungu mingine,
Waisraeli wamejichafua.
11Nawe Yuda vilevile,
nimekupangia wakati utakapovuna azabu.
Currently Selected:
Hosea 6: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Hosea 6
6
Musamaha usiokuwa wa kweli
1Halafu watasema: Tuende tumurudilie Yawe!
Yeye mwenyewe ameturarua,
lakini yeye mwenyewe atatuponyosha.
Yeye mwenyewe ametuumiza,
lakini yeye mwenyewe atatunza vidonda.
2Nyuma ya siku mbili atatupatia tena uzima.
Nyuma ya siku tatu atatufufua
kusudi tuweze kuishi pamoja naye.
3Basi tumutambue,
tujikaze sana kumujua Yawe.
Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko,
yeye atatufikia kama vile manyunyu,
kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.
4Lakini Yawe anasema hivi:
Nitakutendea nini, ee Efuraimu?
Nikufanyie nini, ee Yuda?
Upendo wenu kwangu ni kama ukungu wa asubui,
kama umande unaotoweka upesi.
5Ndiyo maana ninawashambulia kwa njia ya manabii,
nimewaangamiza kwa maneno yangu,
hukumu yangu inajitokeza kama mapambazuko.
6Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka,
kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.
Maovu yanaenea katika inchi yote
7Lakini mulivunja agano langu
kama mulivyofanya katika muji wa Adamu;
kule walikosa uaminifu kwangu.
8Gileadi ni muji wa waovu,
umejaa damu.
9Kama vile wanyanganyi wanavyomuvizia mutu katika njia,
ndivyo makuhani walivyojikusanya na kuvizia.
Wanaua watu katika njia yenye kuelekea Sekemu,
na kutenda uovu mukubwa.
10Nimeona jambo la kuchukiza sana
kati ya Waisraeli:
watu wa Efuraimu wanakimbilia miungu mingine,
Waisraeli wamejichafua.
11Nawe Yuda vilevile,
nimekupangia wakati utakapovuna azabu.
Currently Selected:
:
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.