Waebrania 11:24-27
Waebrania 11:24-27 SWC02
Kwa njia ya imani, Musa alipokuwa mutu muzima, alikataa kuitwa mwana wa binti wa mufalme wa Misri. Alifikiri kwamba ni afazali kuteswa pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika zambi kwa muda mufupi. Aliona kwamba kupatishwa haya kwa ajili ya Kristo kuna faida kubwa zaidi kuliko kupata utajiri wote wa inchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia kupokea zawadi yake. Kwa njia ya imani, Musa alitoka katika inchi ya Misri bila kuogopa kasirani ya mufalme. Na kama vile mutu mwenye kumwona Mungu asiyeonekana, yeye hakurudi nyuma.





