Ezra 2:68-69
Ezra 2:68-69 SWC02
Watu hao waliotoka katika uhamisho, walipofika kwenye nyumba ya Yawe katika Yerusalema, viongozi wamoja wa ukoo hizo walitoa matoleo ya mapenzi kwa kusaidia ujenzi wa nyumba ya Mungu katika Yerusalema. Walitoa kila mutu kadiri ya uwezo wake kwa ajili ya kazi hii. Jumla ya matoleo hayo ilikuwa kilo mia tano za zahabu, kilo elfu mbili na mia nane za feza na nguo mia moja kwa ajili ya makuhani.



