Ezekieli 18:5-9
Ezekieli 18:5-9 SWC02
Kama mutu ni wa haki, ataishi. Mutu wa haki anatenda hivi: anafuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki, hakuli sadaka kwenye milima, haziangalii sanamu za miungu ya Waisraeli, hamuchafui muke wa jirani yake, halali na mwanamuke wakati wake wa ugonjwa wa mwezi, hamutendei mutu yeyote ubaya, anarudisha rehani, haibi, anawapatia wenye njaa chakula anawavalisha wale wanaokuwa uchi, anakopesha bila kudai faida wala kujipatia mazidio, anaepuka kutenda uovu, anaamua kwa haki kati ya mwenye kudai na mwenye kudaiwa, anafuata masharti yangu na kutii maagizo yangu kwa moyo. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.





