Kutoka 2
2
Mutoto Musa anaokotwa katika muto Nili
1Kulikuwa mutu mumoja wa ukoo wa Walawi aliyemuoa mwanamuke mumoja ambaye vilevile alikuwa wa ukoo wa Walawi. 2Basi, mwanamuke yule akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Alipoona kwamba mutoto yule muchanga alikuwa muzuri, akamuficha kwa muda wa miezi mitatu. #Ang. Mdo 7.20; Ebr 11.23 3Lakini kwa vile hakuweza kumuficha zaidi ya muda ule, akatengeneza namna ya kikapu cha mafunjo,#2.3 mafunjo: aina ya majani yanayoota katika muto au katika ziwa. Mabua yake yalitumika hapo kale kwa kutengeneza karatasi (papiro). akakipakaa namna ya kabulimbo, akamutia yule mutoto ndani. Kisha akaweka kikapu kando ya muto Nili katika majani. 4Dada ya yule mutoto akajificha karibu na pahali pale kusudi aone yatakayomupata ndugu yake.
5Basi, binti ya mufalme wa Misri akashuka kwenye muto kuoga na wajakazi wake wakakuwa wanatembeatembea kandokando ya muto. Binti ya mufalme akaona kile kikapu katika majani, akamutuma mujakazi wake akitwae. 6Alipokifungua, akamwona yule mutoto muchanga akilia. Basi, akamwonea huruma, akasema: “Huyu ni mumoja wa watoto wa Waebrania.”
7Palepale dada ya yule mutoto akajitokeza, akamwambia binti ya mufalme: “Niende nikutafutie yaya kati ya wanawake Waebrania akulelee mutoto huyu?”
8Binti ya mufalme akamwambia: “Kwenda.” Basi, yule binti akaenda, akamwita mama ya yule mutoto. 9Binti ya mufalme akamwambia yule mama: “Utunze mutoto huyu, umulee kwa ajili yangu, nami nitakulipa mushahara wako.” Basi, yule mama akamutwaa mutoto, akamulea.
10Mutoto alipokuwa mukubwa, mama yake akamupeleka kwa binti ya mufalme, naye akamutwaa na kumufanya mwana wake. Binti ya mufalme akasema: “Nimemutoa ndani ya maji,” kwa hiyo akamupa mutoto yule jina Musa.#2.10 Musa: Jina “Musa” katika Kiebrania linafanana na neno “mashah” maana yake “kutoa”; lakini jina hilo ni la Kimisri maana yake “Kupata mutoto”. (Linganisha aya hii na Mdo 7.21.)
Musa anakimbilia Midiani
11Siku moja, Musa alipokuwa mutu muzima, akawaendea Waebrania wenzake kwa kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mumisri mumoja akimupiga Mwebrania, mumoja wa wandugu zake. #Ang. Mdo 7.23-28 12Musa akaangalia huku na huko na alipoona kwamba hakuna mutu karibu, akamwua yule Mumisri na kumuficha ndani ya muchanga. 13Kesho yake, Musa akatoka tena, akaona Waebrania wawili wakipigana. Basi, akamwuliza yule aliyekosa: “Kwa nini unamupiga mwenzako?”
14Naye akamujibu: “Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi wetu? Unataka kuniua kama vile ulivyomwua yule Mumisri?”
Kwa hiyo, Musa akaogopa na kufikiri: “Bila shaka jambo hilo limejulikana!” 15Naye mufalme wa Misri aliposikia juu ya tukio hilo akakusudia kumwua Musa. Lakini Musa akamukimbia mufalme, akaenda kukaa katika inchi ya Midiani.#2.15 Midiani: jina la makabila ambayo yalihamahama kwenye eneo la kusini la inchi ya Palestina. Kulingana na Mwa 25.2, Midiani alikuwa mutoto wa Abrahamu.
Siku moja, Musa alikuwa akikaa kando ya kisima cha maji. #Ang. Ebr 11.27 16Basi, wabinti saba wa kuhani mumoja wa kule Midiani wakafika kuchota maji na kuwakunywesha kondoo na mbuzi wa baba yao. 17Wachungaji wengine wakakuja na kuwafukuza wale wabinti. Lakini Musa akawasaidia wabinti wale na kuwakunywesha nyama wao. 18Walipomurudilia baba yao Rueli, yeye akawauliza: “Mbona leo mumerudi upesi hivyo?”
19Nao wakamujibu: “Mumisri mumoja alituokoa toka mikono ya wale wachungaji, naye mwenyewe akachota maji na kuwakunywesha nyama wetu.”
20Baba yao akawauliza wabinti zake: “Yuko wapi? Mbona mumemwacha kule? Mumwite akuje akule chakula.”
21Musa akakubali kukaa kwa yule mutu. Basi, yule mutu akamupa Musa binti yake anayeitwa Zipora akuwe muke wake. 22Zipora akamuzalia mutoto mwanaume. Musa akasema: “Nimekimbilia katika inchi ya kigeni”, kwa hiyo akamupa yule mutoto jina Gersomi.#2.22 Gersomi: maana yake ni “mukimbizi kule”.
Kilio cha Waisraeli katika utumwa
23Nyuma ya muda murefu, mufalme wa Misri akakufa. Waisraeli wakaugua na kulia kutokana na hali yao ya utumwa na kilio chao kikamufikia Mungu juu. 24Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, Isaka, na Yakobo. 25Mungu akawaangalia Waisraeli, naye akatambua hali yao.
Currently Selected:
Kutoka 2: SWC02
Highlight
Share
Copy

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Kutoka 2
2
Mutoto Musa anaokotwa katika muto Nili
1Kulikuwa mutu mumoja wa ukoo wa Walawi aliyemuoa mwanamuke mumoja ambaye vilevile alikuwa wa ukoo wa Walawi. 2Basi, mwanamuke yule akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Alipoona kwamba mutoto yule muchanga alikuwa muzuri, akamuficha kwa muda wa miezi mitatu. #Ang. Mdo 7.20; Ebr 11.23 3Lakini kwa vile hakuweza kumuficha zaidi ya muda ule, akatengeneza namna ya kikapu cha mafunjo,#2.3 mafunjo: aina ya majani yanayoota katika muto au katika ziwa. Mabua yake yalitumika hapo kale kwa kutengeneza karatasi (papiro). akakipakaa namna ya kabulimbo, akamutia yule mutoto ndani. Kisha akaweka kikapu kando ya muto Nili katika majani. 4Dada ya yule mutoto akajificha karibu na pahali pale kusudi aone yatakayomupata ndugu yake.
5Basi, binti ya mufalme wa Misri akashuka kwenye muto kuoga na wajakazi wake wakakuwa wanatembeatembea kandokando ya muto. Binti ya mufalme akaona kile kikapu katika majani, akamutuma mujakazi wake akitwae. 6Alipokifungua, akamwona yule mutoto muchanga akilia. Basi, akamwonea huruma, akasema: “Huyu ni mumoja wa watoto wa Waebrania.”
7Palepale dada ya yule mutoto akajitokeza, akamwambia binti ya mufalme: “Niende nikutafutie yaya kati ya wanawake Waebrania akulelee mutoto huyu?”
8Binti ya mufalme akamwambia: “Kwenda.” Basi, yule binti akaenda, akamwita mama ya yule mutoto. 9Binti ya mufalme akamwambia yule mama: “Utunze mutoto huyu, umulee kwa ajili yangu, nami nitakulipa mushahara wako.” Basi, yule mama akamutwaa mutoto, akamulea.
10Mutoto alipokuwa mukubwa, mama yake akamupeleka kwa binti ya mufalme, naye akamutwaa na kumufanya mwana wake. Binti ya mufalme akasema: “Nimemutoa ndani ya maji,” kwa hiyo akamupa mutoto yule jina Musa.#2.10 Musa: Jina “Musa” katika Kiebrania linafanana na neno “mashah” maana yake “kutoa”; lakini jina hilo ni la Kimisri maana yake “Kupata mutoto”. (Linganisha aya hii na Mdo 7.21.)
Musa anakimbilia Midiani
11Siku moja, Musa alipokuwa mutu muzima, akawaendea Waebrania wenzake kwa kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mumisri mumoja akimupiga Mwebrania, mumoja wa wandugu zake. #Ang. Mdo 7.23-28 12Musa akaangalia huku na huko na alipoona kwamba hakuna mutu karibu, akamwua yule Mumisri na kumuficha ndani ya muchanga. 13Kesho yake, Musa akatoka tena, akaona Waebrania wawili wakipigana. Basi, akamwuliza yule aliyekosa: “Kwa nini unamupiga mwenzako?”
14Naye akamujibu: “Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi wetu? Unataka kuniua kama vile ulivyomwua yule Mumisri?”
Kwa hiyo, Musa akaogopa na kufikiri: “Bila shaka jambo hilo limejulikana!” 15Naye mufalme wa Misri aliposikia juu ya tukio hilo akakusudia kumwua Musa. Lakini Musa akamukimbia mufalme, akaenda kukaa katika inchi ya Midiani.#2.15 Midiani: jina la makabila ambayo yalihamahama kwenye eneo la kusini la inchi ya Palestina. Kulingana na Mwa 25.2, Midiani alikuwa mutoto wa Abrahamu.
Siku moja, Musa alikuwa akikaa kando ya kisima cha maji. #Ang. Ebr 11.27 16Basi, wabinti saba wa kuhani mumoja wa kule Midiani wakafika kuchota maji na kuwakunywesha kondoo na mbuzi wa baba yao. 17Wachungaji wengine wakakuja na kuwafukuza wale wabinti. Lakini Musa akawasaidia wabinti wale na kuwakunywesha nyama wao. 18Walipomurudilia baba yao Rueli, yeye akawauliza: “Mbona leo mumerudi upesi hivyo?”
19Nao wakamujibu: “Mumisri mumoja alituokoa toka mikono ya wale wachungaji, naye mwenyewe akachota maji na kuwakunywesha nyama wetu.”
20Baba yao akawauliza wabinti zake: “Yuko wapi? Mbona mumemwacha kule? Mumwite akuje akule chakula.”
21Musa akakubali kukaa kwa yule mutu. Basi, yule mutu akamupa Musa binti yake anayeitwa Zipora akuwe muke wake. 22Zipora akamuzalia mutoto mwanaume. Musa akasema: “Nimekimbilia katika inchi ya kigeni”, kwa hiyo akamupa yule mutoto jina Gersomi.#2.22 Gersomi: maana yake ni “mukimbizi kule”.
Kilio cha Waisraeli katika utumwa
23Nyuma ya muda murefu, mufalme wa Misri akakufa. Waisraeli wakaugua na kulia kutokana na hali yao ya utumwa na kilio chao kikamufikia Mungu juu. 24Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, Isaka, na Yakobo. 25Mungu akawaangalia Waisraeli, naye akatambua hali yao.
Currently Selected:
:
Highlight
Share
Copy

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.