YouVersion Logo
Search Icon

Danieli 7

7
Nyama wane wakubwa
1Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa mufalme Belsasari wa Babeli, Danieli aliota ndoto na kuona maono akiwa amelala katika kitanda chake. Akaandika ndoto yake hii:
2Mimi Danieli niliona maono usiku. Ilikuwa hivi: Upepo ulivuma juu ya bahari kubwa toka pande zote ine za mbinguni. 3Nyama wakubwa wane wakainuka kutoka ndani ya bahari, kila mumoja akiwa tofauti na mwenzake. #Ang. Ufu 13.1; 17.8 4Nyama wa kwanza alikuwa kama simba, na alikuwa na mabawa kama ya tai. Nikiwa ninamwangalia, mabawa yake yaliongolewa, naye akainuliwa na kusimama kwa miguu miwili kama mutu. Kisha, akapewa akili ya kimutu. #Ang. Ufu 13.2
5Nyama wa pili alikuwa kama dubu ambaye upande wake mumoja ulikuwa umeinuka. Na katika kinywa chake alikuwa na mifupa mitatu ya mbavu aliyoishika kwa meno yake. Sauti ikamwambia: Simama, ukule nyama nyingi kadiri unavyoweza.
6Nyuma ya mambo hayo, nikaona nyama mwingine. Huyu alikuwa kama chui mwenye mabawa mane ya ndege juu ya mugongo wake. Alikuwa na vichwa vine naye alipewa uwezo wa kutawala.
7Kisha, katika maono hayo yangu ya usiku, nikaona nyama wa ine wa ajabu na wa kutisha, mwenye nguvu sana. Huyu alikuwa na meno makubwa ya chuma ambayo aliyatumia kwa kula na kuvunjavunja, na mabaki aliyakanyagakanyaga. Alikuwa tofauti na wale nyama wengine watatu, maana alikuwa na pembe kumi. #Ang. Ufu 12.3; 13.1 8Nilipokuwa ninaziangalia hizo pembe, niliona pembe ingine ndogo ikiota katikati ya zile kumi, nayo ikaongoa pembe tatu kati ya hizo za kwanza. Pembe ile ilikuwa na macho ya kimutu na kinywa kilichosema maneno ya kujivuna. #Ang. Ufu 13.5-6
Kuangamizwa kwa nyama wale
9Nilipokuwa nikiendelea kuangalia, nikaona viti vya kifalme viliwekwa hapo, kisha Muzee mumoja wa zamani sana akakuja, akaikaa. Alikuwa amevaa nguo nyeupe kama teluji; nywele zake zilikuwa kama sufu safi. Kiti chake cha kifalme kilikuwa ndimi za moto, na magurudumu ya kiti kile yalikuwa moto unaowaka. #Ang. Ufu 20.4; 1.14 10Kutoka kiti hicho kijito cha moto kilibubujika, kikatiririka. Maelfu ya watu walimutumikia, na mamilioni walisimama mbele yake. Halafu waamuzi wakajitayarisha kwa kuhukumu, na vitabu vikafunguliwa. #Ang. Ufu 5.11; 20.12
11Kutokana na maneno ya kujivuna yaliyokuwa yanasemwa na ile pembe, nikaendelea kuangalia. Nikaona yule nyama wa ine akiuawa, mwili wake ukaharibiwa na kutolewa uchomwe kwa moto. 12Wale nyama wengine walinyanganywa mamlaka yao, lakini wao wenyewe wakaachwa waendelee kuishi kwa muda fulani.
13Wakati wa maono haya usiku, niliona kiumbe kinachofanana na mwanadamu. Akakuja katika mawingu na kumwendea yule Muzee wa zamani sana. Akakaribishwa mbele yake. #Ang. Mat 24.30; 26.64; Mk 13.26; Lk 21.27; Ufu 1.7; 14.14 14Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme, kusudi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote wamutumikie. Utawala wake ni wa milele na ufalme wake hautaangamizwa hata kidogo. #Ang. Ufu 11.15
Maelezo ya maono ya kwanza
15Maono niliyoyaona mimi Danieli yaliniogopesha, nami nikafazaika. 16Nikajongea karibu na mutu mumoja kati ya wale waliosimama pale na kumwuliza maana kamili ya mambo hayo yote. Naye akanielezea maana yake akisema: 17Nyama hao wane wakubwa ni wafalme wane watakaotokea katika dunia. 18Lakini watakatifu wa Mungu Mukubwa watapewa ufalme, nao wataupokea ufalme huo milele na milele. #Ang. Ufu 22.5
19Kisha nikataka nielezwe juu ya yule nyama wa ine, ambaye alikuwa tofauti kabisa na wale wengine, wa kutisha sana, mwenye meno ya chuma na makucha ya shaba, aliyekula na kuvunjavunja, na kukanyagakanyaga yaliyobaki. 20Vilevile nilitaka nielezwe juu ya zile pembe kumi alizokuwa nazo juu ya kichwa chake, na ile pembe moja iliyoota na pembe zingine tatu zilizoanguka mbele yake, ndiyo ile pembe iliyokuwa na macho na kinywa ambacho kilisema maneno ya kujivuna, na ambayo ilionekana kuwa kubwa kuliko pembe zingine.
21Nilipokuwa nikiangalia, pembe hio ilipigana vita na watakatifu, nayo ikawashinda. #Ang. Ufu 13.7 22Lakini yule Muzee wa zamani sana akainuka, akawapa haki watakatifu wa Mungu na wakati ulipotimia, hao watakatifu wakapewa ufalme. #Ang. Ufu 20.4
23Nilielezwa hivi: Yule nyama wa ine ni ufalme wa ine utakaokuwa katika dunia. Ufalme huo utakuwa tofauti na falme zingine, nao utaiangamiza dunia nzima. Utaiangusha chini na kuipasua vipandevipande. 24Zile pembe kumi ni wafalme kumi watakaotokana na ufalme huo. Halafu watafuatwa na mufalme mwingine ambaye atakuwa tofauti na wale waliomutangulia, na atawaangusha wafalme watatu. #Ang. Ufu 17.12 25Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu. #Ang. Ufu 12.14; 13.5-6 26Lakini waamuzi watajitayarisha kwa kuamua watamunyanganya utawala wake, nao utafutwa na kuangamizwa kabisa. 27Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.
28Huu ndio mwisho wa jambo hilo. Mawazo yangu yaliniogopesha sana mimi Danieli, hata rangi yangu ikabadilika. Lakini nilichunga jambo hilo ndani ya moyo wangu.

Currently Selected:

Danieli 7: SWC02

Highlight

Share

Compare

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in