1 Samweli 28:7-8
1 Samweli 28:7-8 SWC02
Halafu Saulo akawaambia watumishi wake: “Munitafutie mwanamuke ambaye anaweza kuaguza kusudi nimwendee na kumwomba shauri.” Watumishi wake wakamujibu: “Kuna mwanamuke mwaguzi mumoja kule Endori.” Basi, Saulo akajigeuza na kuvaa nguo zingine, akaenda kule pamoja na watu wake wawili. Walifika kwa yule mwanamuke usiku. Saulo akamwambia: “Unifanyie uaguzi na kunipandishia mutu yeyote nitakayekutajia.”





