YouVersion Logo
Search Icon

Mk 10:1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 11, 12, 13, 14, 15, 16, 17, 18, 19, 20, 21, 22, 23, 24, 25, 26, 27, 28, 29, 30, 31

Mk 10:2 SUV

Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamwuliza, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe? Huku wakimjaribu.

Mk 10:3 SUV

Naye akajibu, akawaambia, Musa aliwaamuru nini?

Mk 10:4 SUV

Wakasema, Musa alitoa ruhusa kuandika hati ya talaka na kumwacha.

Mk 10:5 SUV

Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii.

Mk 10:6 SUV

Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.

Mk 10:7 SUV

Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe

Mk 10:8 SUV

na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.

Mk 10:9 SUV

Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.

Mk 10:11 SUV

Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake

Mk 10:12 SUV

na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini.

Mk 10:13 SUV

Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea.

Mk 10:15 SUV

Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.

Mk 10:16 SUV

Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia.

Mk 10:18 SUV

Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu.

Mk 10:20 SUV

Akamwambia, Mwalimu, haya yote nimeyashika tangu utoto wangu.

Mk 10:25 SUV

Ni rahisi ngamia kupenya katika tundu ya sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.

Mk 10:26 SUV

Nao wakashangaa mno, wakimwambia, Ni nani, basi, awezaye kuokoka?

Mk 10:28 SUV

Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe.

Mk 10:31 SUV

Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho; na wa mwisho watakuwa wa kwanza.

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy