YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 120

120
Zaburi 120
Kuomba Msaada
Wimbo wa kwenda juu.
1 Katika dhiki yangu namwita Bwana,
naye hunijibu.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo
na ndimi za udanganyifu.
3Atakufanyia nini,
au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,
kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki,
kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6Nimeishi muda mrefu mno
miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7Mimi ni mtu wa amani;
lakini ninaposema, wao wanataka vita.

Currently Selected:

Zaburi 120: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy