YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 118

118
Zaburi 118
Shukrani Kwa Ajili Ya Ushindi
1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema;
upendo wake wadumu milele.
2 Israeli na aseme sasa:
“Upendo wake wadumu milele.”
3 Nyumba ya Aroni na iseme sasa:
“Upendo wake wadumu milele.”
4 Wote wamchao Bwana na waseme sasa:
“Upendo wake wadumu milele.”
5 Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana,
naye akanijibu kwa kuniweka huru.
6 Bwana yuko pamoja nami, sitaogopa.
Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
7 Bwana yuko pamoja nami,
yeye ni msaidizi wangu.
Nitawatazama adui zangu
wakiwa wameshindwa.
8 Ni bora kumkimbilia Bwana
kuliko kumtumainia mwanadamu.
9 Ni bora kumkimbilia Bwana
kuliko kuwatumainia wakuu.
10 Mataifa yote yalinizunguka,
lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
11 Walinizunguka pande zote,
lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
12 Walinizunguka kama kundi la nyuki,
lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo;
kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
13 Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka,
lakini Bwana alinisaidia.
14 Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu,
yeye amefanyika wokovu wangu.
15 Sauti za shangwe na ushindi
zinavuma hemani mwa wenye haki:
“Mkono wa kuume wa Bwana
umetenda mambo makuu!
16 Mkono wa kuume wa Bwana
umeinuliwa juu,
mkono wa kuume wa Bwana
umetenda mambo makuu!”
17 Sitakufa, bali nitaishi,
nami nitatangaza yale Bwana aliyoyatenda.
18 Bwana ameniadhibu vikali,
lakini hakuniacha nife.
19 Nifungulie malango ya haki,
nami nitaingia na kumshukuru Bwana.
20 Hili ni lango la Bwana
ambalo wenye haki wanaweza kuliingia.
21 Nitakushukuru, kwa kuwa ulinijibu,
umekuwa wokovu wangu.
22 Jiwe walilolikataa waashi,
limekuwa jiwe kuu la pembeni.
23 Bwana ametenda hili,
nalo ni la kushangaza machoni petu.
24 Hii ndiyo siku Bwana aliyoifanya,
tushangilie na kufurahi ndani yake.
25 Ee Bwana, tuokoe,
Ee Bwana, utujalie mafanikio.
26 Heri yule ajaye kwa jina la Bwana.
Kutoka nyumba ya Bwana tunakubariki.
27 Bwana ndiye Mungu,
naye ametuangazia nuru yake.
Mkiwa na matawi mkononi,
unganeni kwenye maandamano ya sikukuu
hadi kwenye pembe za madhabahu.
28 Wewe ni Mungu wangu, nitakushukuru,
wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza.
29Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema;
upendo wake wadumu milele.

Currently Selected:

Zaburi 118: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy