YouVersion Logo
Search Icon

3 Yohana Utangulizi

Utangulizi
Waraka wa tatu wa Yohana uliandikiwa Gayo, ambaye alikuwa kiongozi muhimu katika kanisa. Alielekezwa kuwasaidia na kuwahudumia wale waliokuja kama wajumbe wa Mungu. Pia alipewa onyo kuhusu Deotrefe, juu ya tabia yake ya kukosa ushirikiano. Yohana alieleza tarajio lake la kuja na kushughulikia tatizo hili mwenyewe.
Mwandishi
Mtume Yohana.
Kusudi
Yohana anamwandikia Gayo akimpa onyo kuhusu Deotrefe, kwa tabia yake ya kukosa ushirikiano.
Mahali
Efeso.
Tarehe
Kama mwaka wa 90 B.K.
Wahusika Wakuu
Yohana, Gayo, Deotrefe, na Demetrio.
Wazo Kuu
Wajibu binafsi wa Gayo kuhusu watumishi wa kweli na wa uongo.
Mambo Muhimu
Yohana anamtakia Gayo kufanikiwa katika mambo yote, na pia anamwagiza asiige lililo baya bali aige lililo jema.
Mgawanyo
Salamu (1-4)
Kutiwa moyo kwa Gayo (5-8)
Kukemewa kwa Deotrefe (9-10)
Kusifiwa kwa Demetrio (11-12)
Hitimisho (13-14).

Currently Selected:

3 Yohana Utangulizi: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy