1
Mathayo 14:30-31
Neno: Maandiko Matakatifu 2024
NENO
Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu, naye akaanza kuzama, akapaza sauti na kusema, “Bwana, niokoe!” Mara Isa akaunyoosha mkono wake na kumshika, akamwambia, “Wewe mwenye imani haba, kwa nini uliona shaka?”
Compare
Explore Mathayo 14:30-31
2
Mathayo 14:30
Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu, naye akaanza kuzama, akapaza sauti na kusema, “Bwana, niokoe!”
Explore Mathayo 14:30
3
Mathayo 14:27
Lakini mara Isa akasema nao, akawaambia, “Jipeni moyo! Ni mimi. Msiogope.”
Explore Mathayo 14:27
4
Mathayo 14:28-29
Petro akamjibu, “Bwana Isa, ikiwa ni wewe, niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.” Isa akamwambia, “Njoo.” Basi Petro akatoka kwenye chombo, akatembea juu ya maji kumwelekea Isa.
Explore Mathayo 14:28-29
5
Mathayo 14:33
Ndipo wote waliokuwa ndani ya ile mashua wakamwabudu Isa, wakisema, “Hakika, wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
Explore Mathayo 14:33
6
Mathayo 14:16-17
Isa akawaambia, “Hakuna sababu ya wao kuondoka. Ninyi wapeni chakula.” Wakamjibu, “Tuna mikate mitano na samaki wawili tu.”
Explore Mathayo 14:16-17
7
Mathayo 14:18-19
Akawaambia, “Nileteeni hivyo vitu hapa.” Isa akaagiza umati wa watu wakae chini kwenye nyasi. Akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akainua macho yake akatazama mbinguni, akavibariki na kuimega ile mikate. Kisha akawapa wanafunzi, nao wanafunzi wakawagawia ule umati.
Explore Mathayo 14:18-19
8
Mathayo 14:20
Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
Explore Mathayo 14:20