1
Yoshua 2:11
Neno: Maandiko Matakatifu 2024
NENO
Tuliposikia kuhusu hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ni Mungu juu mbinguni na chini duniani.
Compare
Explore Yoshua 2:11
2
Yoshua 2:10
Tumesikia jinsi Mwenyezi Mungu alivyokausha maji ya Bahari ya Shamu kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki mwa Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa.
Explore Yoshua 2:10
3
Yoshua 2:8-9
Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini, akawaambia, “Ninajua kuwa Mwenyezi Mungu amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote wanaoishi katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
Explore Yoshua 2:8-9
Home
Bible
Plans
Videos