Basi, ukuta ikamalizika siku ya makumi mbili na tano ya mwezi wa Eluli; nayo ilidumu muda wa siku makumi tano na mbili. Waadui zetu katika mataifa jirani, waliposikia kwamba kazi tumeimaliza, wakaogopa na kupata haya sana; maana walijua hakika kwamba kazi hii ilikamilika kwa musaada wa Mungu wetu.