1
Luka 2:11
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Leo hii Mwokozi amezaliwa kwa ajili yenu katika muji wa Daudi, yeye ndiye Kristo na Bwana.
Compare
Explore Luka 2:11
2
Luka 2:10
Lakini malaika akawaambia: “Musiogope, kwa sababu ninawaletea Habari Njema itakayofurahisha sana watu wote.
Explore Luka 2:10
3
Luka 2:14
“Sifa kwa Mungu juu mbinguni, na amani katika dunia kwa watu anaowapenda.”
Explore Luka 2:14
4
Luka 2:52
Na Yesu alizidi kuwa na hekima, na kuongezeka kimo na kuendelea kumupendeza Mungu na watu.
Explore Luka 2:52
5
Luka 2:12
Na hiki ndicho kitambulisho kwenu: mutamukuta mutoto muchanga amefunikwa nguo za kitoto, naye amelalishwa katika sanduku ya kukulishia nyama.”
Explore Luka 2:12
6
Luka 2:8-9
Na katika pande zile, kulikuwa wachungaji kule katika mbuga wakichunga kondoo zao usiku. Na kwa rafla malaika wa Bwana akawatokea, na mwangaza wa utukufu wa Bwana ukawazunguka. Nao wakaogopa sana.
Explore Luka 2:8-9
Home
Bible
Plans
Videos