Mungu, kwa nguvu yake, anawaangamiza wenye uwezo;
anasimama, nao wanakata tamaa ya kuishi.
Anawaacha waovu wajione salama,
lakini macho yake yanachunguza mienendo yao.
Waovu wanafanikiwa kwa muda tu, kisha wanatoweka,
wananyauka na kufifia kama vile jani,
wanakatwa kama vile masuke ya ngano.