Hili ni neno Yawe alilomwambia nabii Yeremia juu ya Wafilistini, mbele mufalme wa Misri hajaushambulia muji wa Gaza:
Yawe anasema hivi:
Maji yanapanda kutoka kaskazini,
nayo yatakuwa muto uliofurika;
yataifunika inchi nzima na vyote vinavyokuwa ndani yake,
muji na wakaaji na wanaoishi humo.
Watu watalia,
wakaaji wote wa inchi wataomboleza.