Wewe, kubali tu kosa lako:
kwamba umeniasi mimi Yawe, Mungu wako;
kwamba chini ya kila muti wenye majani,
umeonyesha mapenzi yako kwa miungu mingine,
wala haukuitii sauti yangu.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu,
maana, mimi ndimi Bwana wenu.
Nitawatwaa mumoja kutoka kila muji,
na wawili kutoka katika kila ukoo,
niwapeleke mpaka kwenye mulima Sayuni.
–Ni ujumbe wa Yawe.