Kila mara ninaposema kitu, ninalalamika,
ninapandisha sauti kwa kutangaza mateso na uharibifu.
Kutangaza neno la Yawe kunaniletea
kuzomewa na kuzarauliwa kila siku.
Lakini ninaposema “Sitamutaja tena Yawe,
wala sitasema tena kwa jina lake”,
ndani yangu kunawaka kitu kama moto
uliofungiwa ndani ya mifupa yangu.
Ninajaribu sana kuuzuia humo,
lakini ninashindwa.