Kisha watu wakavishika vivuko vya muto Yordani kwa kuiziba njia ya watu wa Efuraimu. Kila mara mukimbizi alipotokea akiomba kupita kule, watu wa Gileadi walimwuliza: “Wewe ni Mwefuraimu?” Na kama akijibu “Hapana”, walimwambia: “Basi useme neno ‘Shiboleti’ ”. Lakini yeye akisema “Siboleti” kwa sababu hakuweza kulitamka sawasawa, walimukamata na kumwua kule kwenye vivuko vya muto Yordani. Watu elfu makumi ine na mbili wa Efuraimu wakapoteza maisha yao wakati ule.