1
Isaya 65:24
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Hata mbele hawajaniita, mimi nitawaitikia; mbele hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.
Compare
Explore Isaya 65:24
2
Isaya 65:17
Sasa, ninaumba mbingu mupya na dunia mupya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa tena.
Explore Isaya 65:17
3
Isaya 65:23
Kazi zao hazitakuwa bure, wala hawatazaa watoto watakaopatwa na musiba; maana watakuwa waliobarikiwa na Yawe, wamebarikiwa wao pamoja na wazao wao.
Explore Isaya 65:23
4
Isaya 65:22
Hawatajenga nyumba na watu wengine wakae ndani yake, wala kulima chakula kikuliwe na watu wengine. Maana watu wangu niliowachagua wataishi maisha marefu kama miti; wachaguliwa wangu watafurahia matunda ya jasho lao.
Explore Isaya 65:22
5
Isaya 65:20
Hakutakuwa tena vifo vya watoto wachanga, wazee nao hawatakufa mbele ya wakati wao. Mutu wa miaka mia moja akikufa, amekufa akiwa kijana; na akikufa mbele ya miaka mia moja, ni kusema amelaaniwa.
Explore Isaya 65:20
6
Isaya 65:25
Imbwa wa pori na kondoo watakula pamoja, simba watakula majani kama ngombe, lakini chakula cha nyoka kitakuwa mavumbi. Katika mulima wangu wote mutakatifu, hakuna atakayeumiza au kuharibu kitu. –Ni Yawe anayesema hivyo.
Explore Isaya 65:25
7
Isaya 65:19
Nami nitaufurahia Yerusalema, nitawafurahia watu wangu. Sauti ya kilio haitasikilika tena, kilio cha taabu hakitakuwa tena.
Explore Isaya 65:19