1
Ezekieli 34:16
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.
Compare
Explore Ezekieli 34:16
2
Ezekieli 34:12
Kama muchungaji anavyowatafuta kondoo wake waliosambazwa, ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawarudisha kutoka kila pahali waliposambazwa kwa siku yenye mawingu ya hatari na giza nene.
Explore Ezekieli 34:12
3
Ezekieli 34:11
Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo wangu na kuwatunza.
Explore Ezekieli 34:11
4
Ezekieli 34:15
Mimi mwenyewe nitakuwa muchungaji wa kondoo wangu. Mimi mwenyewe nitawapumzisha. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Explore Ezekieli 34:15
5
Ezekieli 34:31
Nanyi, ee kondoo wangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Explore Ezekieli 34:31
6
Ezekieli 34:2
Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya wachungaji wa inchi ya Israeli. Uwaambie hao wachungaji kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ole kwenu ninyi wachungaji wa inchi ya Israeli, munaojikulisha ninyi wenyewe tu! Haiwapasi wachungaji kuwakulisha kondoo?
Explore Ezekieli 34:2