Kisha Yawe akapita mbele ya Musa akitangaza tena:
Yawe, Yawe,
ni Mungu mwenye rehema na huruma,
si mwepesi wa hasira,
ni mwingi wa wema na uaminifu.
Anawatendea mema maelfu,
anawasamehe uovu, makosa na zambi.
Lakini hataacha kumwazibu mwenye kosa.
Anawalipiza watoto na wajukuu
uovu wa baba na babu zao,
hata kizazi cha tatu na cha ine.