Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi kwa ajili ya taa, kuwe taa inayowaka siku zote. Hiyo itakuwa ndani ya hema la mukutano inje ya pazia lile mbele ya Sanduku la Agano na Haruni na wana wake wataitunza mbele yangu tangu magaribi mpaka asubui. Sharti hili lifuatwe siku zote na Waisraeli wote, kizazi kwa kizazi.