Haya ni maneno ya Amosi, mumoja wa wachungaji wa nyama wa muji wa Tekoa. Mungu alimufunulia Amosi mambo haya yote juu ya inchi ya Israeli miaka miwili mbele ya tetemeko la inchi, wakati Uzia alipokuwa mufalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi alipokuwa mufalme wa Israeli. Amosi alisema hivi:
Yawe ananguruma toka mulima Sayuni,
anavumisha sauti yake toka Yerusalema,
hata mashamba ya malisho ya wachungaji yanakauka,
majani ya mulima Karmeli yananyauka.