Kisha kukaa pamoja nao muda wa siku nane au kumi, Festo akarudi Kaisaria. Kesho yake akaikaa ndani ya tribinali na kuamuru wamulete Paulo. Wakati Paulo alipofika, wale Wayuda waliotoka Yerusalema wakamuzunguka na kutoa mashitaki mengi mazito juu yake ambayo wao hawawezi kuhakikisha.