Mungu ndiye anayemupatia mupandaji mbegu na mukate wa kukula. Kwa hiyo atawapatia ninyi mbegu yoyote munayohitaji na kuiotesha, kusudi moyo wenu wa kutoa upate kuzaa matunda mengi. Hivi mutakuwa watajiri katika vitu vyote, kusudi siku zote muweze kuonyesha moyo wa kutoa, hata watu wengi watamushukuru Mungu kwa ajili ya musaada tunaowafikishia kutoka kwenu.