1
2 Wakorinto 4:18
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Maana sisi hatuangalii vitu vile vinavyoonekana, lakini vitu visivyoonekana. Kwa sababu vile vinavyoonekana vinadumu muda kidogo tu, lakini vile visivyoonekana, vinadumu milele.
Compare
Explore 2 Wakorinto 4:18
2
2 Wakorinto 4:16-17
Kwa sababu hii hatukati tumaini hata kidogo. Ijapokuwa hali yetu ya kimwili inaharibika, hali yetu ya kiroho inafanywa upya siku kwa siku. Kwa maana taabu tunayopata ni ndogo na ya muda tu, inatutayarishia utukufu mukubwa sana na wa milele unaokuwa muzuri zaidi kupita mateso haya.
Explore 2 Wakorinto 4:16-17
3
2 Wakorinto 4:8-9
Sisi tunagandamizwa kila namna, lakini hatushindwi; tunahangaishwa, lakini hatukati tumaini; tunateswa, lakini Mungu hatuachilii; tunatupwa chini, lakini hatuangamizwi.
Explore 2 Wakorinto 4:8-9
4
2 Wakorinto 4:7
Lakini sisi tunaokuwa na hazina hii ya kiroho, tuko vyombo vya udongo, kusudi watu waone waziwazi uwezo huu wa ajabu sana unaotoka kwa Mungu lakini si kwetu sisi wenyewe.
Explore 2 Wakorinto 4:7
5
2 Wakorinto 4:4
Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.
Explore 2 Wakorinto 4:4
6
2 Wakorinto 4:6
Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.
Explore 2 Wakorinto 4:6
Home
Bible
Plans
Videos