Waimbaji na wapiga baragumu wote pamoja walitoa sauti kwa pamoja na matoazi na vyombo vingine vya muziki, wakimusifu Yawe wakiimba: “Yeye ni muzuri. Wema wake unadumu milele.” Wakati ule nyumba ya Yawe ikajazwa na wingu. Nao makuhani walishindwa kutumika kwa sababu ya wingu lile, maana utukufu wa Yawe ulijaza nyumba ya Mungu.