Watu wa Daudi wakamwambia: “Ile siku Yawe aliyokuambia kwamba atakuja kumutia adui yako katika mikono yako nawe umutendee utakavyoona inafaa, leo imefika.”
Halafu Daudi alimwendea Saulo polepole kutoka nyuma, akakata pindo la nguo yake. Daudi akaanza kufazaika ndani ya moyo kwa sababu alikata pindo la nguo ya Saulo kwa siri.