Soma Biblia Kila Siku Mei 2021预览

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021

31天中的第25天

Nyakati nyingi wanadamu hujivuna wakijihesabu kuwa wanao uwezo wa kuamua na kutenda watakacho. Moyo wa namna hii hujawa na kiburi na kujikweza. Nyuma ya pazia la moyo huo ni Ibilisi autawalaye utashi wake. Mungu amtazamapo mtu huyu, humwita mpumbavu kwa kutotambua alivyo maskini na mkiwa. Hana lolote awezalo kutenda. Si kwamba twatosha sisi wenyewe kufikiri neno lolote kwamba ni letu wenyewe, bali utoshelevu wetu watoka kwa Mungu (2 Kor 3:5). Kwa hiyo tumnyenyekee Mungu atuwezesheaye.

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ayubu. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu

More