Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021预览

Kuna wanadamu wawili wenye maana sana kwetu. Ni Adamu mwenye dhambi na Kristo Yesu mtakatifu, asiye mdhambi. Kristo ni zawadi ya ajabu kwa ajili yetu tulio wenye dhambi kama Adamu. Kwa kuwa Kristo ni asili ya msamaha, upatanisho na amani, ni mwanzo wa kufufuka kwa wote wanaomwamini Yeye. Ni kweli, Lazaro alifufuliwa na Yesu. Lakini Lazaro hakuishi milele. Ni Kristo tu aliyekufa na anaishi leo. Yeye hafi tena. Tayari anatawala, na siku moja ataangamiza adui wa mwisho ambaye ni kifo.