Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021预览

Baada ya kifo cha Yesu, wanafunzi wake waliishi kwa mashaka na hofu ya kuwaogopa Wayahudi. Lakini kufufuka kwa Yesu kuliwaletea tumaini la maisha mapya kimwili na kiroho. Siku hizi tunamhubiri Kristo kwamba yu hai, kwani alifufuka; na kama alivyojifunua kwa wanafunzi, leo yupo kwetu kutuokoa na kutusamehe dhambi zetu. Pia kufufuka kwa Yesu kunatuhakikishia ndiye Mwana wa Mungu, na kunatupa tumaini letu la kufufuka siku ya mwisho. Mkaribishe Yesu aliyefufuka moyoni mwako ili ashughulike na maisha yako, nawe utaona baraka zake.