Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Tafuta matokeo ya: strength

Flp 4:13 (SUV)

Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

2 Kor 12:9 (SUV)

Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.

Efe 6:10 (SUV)

Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.

Isa 40:31 (SUV)

bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.

Isa 41:10 (SUV)

usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

Yos 1:9 (SUV)

Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.

Efe 6:11 (SUV)

Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

1 Pet 5:10 (SUV)

Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.

Efe 3:17 (SUV)

Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani mkiwa na shina na msingi katika upendo;

Efe 3:18 (SUV)

ili mpate kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina;

Efe 3:19 (SUV)

na kuujua upendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, mpate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu.

Zab 27:14 (SUV)

Umngoje BWANA, uwe hodari, Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.

Efe 6:12 (SUV)

Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

Efe 6:13 (SUV)

Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

Efe 6:14 (SUV)

Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

Efe 6:16 (SUV)

zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

Efe 6:17 (SUV)

Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;

2 Tim 1:7 (SUV)

Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.

Yak 1:2 (SUV)

Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;

Yak 1:3 (SUV)

mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.

1 Pet 5:9 (SUV)

Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.

Rum 5:3 (SUV)

Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi;

Rum 5:4 (SUV)

na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;

1 Kor 10:13 (SUV)

Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

Efe 6:15 (SUV)

na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;