Tafuta matokeo ya: strength
Flp 4:13 (SUV)
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
2 Kor 12:9 (SUV)
Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
Efe 6:10 (SUV)
Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.
Isa 40:31 (SUV)
bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
Isa 41:10 (SUV)
usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
Yos 1:9 (SUV)
Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.
Efe 6:11 (SUV)
Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
1 Pet 5:10 (SUV)
Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.
Efe 3:17 (SUV)
Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani mkiwa na shina na msingi katika upendo;
Efe 3:18 (SUV)
ili mpate kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina;
Efe 3:19 (SUV)
na kuujua upendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, mpate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu.
Zab 27:14 (SUV)
Umngoje BWANA, uwe hodari, Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.
Efe 6:12 (SUV)
Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
Efe 6:13 (SUV)
Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
Efe 6:14 (SUV)
Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
Efe 6:16 (SUV)
zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
Efe 6:17 (SUV)
Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;
2 Tim 1:7 (SUV)
Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.
Yak 1:2 (SUV)
Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;
Yak 1:3 (SUV)
mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
1 Pet 5:9 (SUV)
Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.
Rum 5:3 (SUV)
Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi;
Rum 5:4 (SUV)
na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;
1 Kor 10:13 (SUV)
Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.
Efe 6:15 (SUV)
na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;