Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Tafuta matokeo ya: purity

1 Tim 4:12 (SUV)

Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.

Zab 119:9 (SUV)

Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.

1 Kor 6:19 (SUV)

Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

1 Kor 6:20 (SUV)

maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yen

Flp 4:8 (SUV)

Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.

Zab 51:10 (SUV)

Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu

2 Kor 7:1 (SUV)

Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.

1 The 4:3 (SUV)

Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;

1 The 4:4 (SUV)

kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;

1 Kor 6:18 (SUV)

Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.

Efe 5:3 (SUV)

Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;

1 The 4:5 (SUV)

si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu.

1 The 4:7 (SUV)

Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.

1 The 4:8 (SUV)

Basi yeye anayekataa, hakatai mwanadamu bali Mungu, anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.

2 Tim 2:22 (SUV)

Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.

Zab 119:11 (SUV)

Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.

Ebr 4:16 (SUV)

Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.

Yak 1:14 (SUV)

Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.

Yak 1:21 (SUV)

Kwa hiyo wekeeni mbali uchafu wote na ubaya uzidio, na kupokea kwa upole neno lile lililopandwa ndani, liwezalo kuziokoa roho zenu.

Yak 4:7 (SUV)

Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.

Yak 4:8 (SUV)

Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.

Yak 5:16 (SUV)

Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

1 Pet 5:8 (SUV)

Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.

1 Pet 5:9 (SUV)

Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.

1 Yoh 1:9 (SUV)

Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.